Skip to main content
Mwenyekiti
Contact Info
Education

Ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi tangu mwaka 2018. Katika nafasi hiyo, mtazamo wake ni kubuni mikakati na sera za Kampuni, kuimarisha uongozi, na kukidhi matakwa ya wanahisa. Hivi sasa Bwana Magambo ni Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji wa Mfuko wa PSSSF na anauwakilisha Mfuko huo kwenye Bodi. Ni Mjumbe wa Bodi wa Nguru Hills Ranch Ltd, Benki ya Posta na  Ubungo Plaza Ltd. Ana uzoefu kwenye maeneo yafuatayo:-  Utawala, Uongozi, Mashirika, Usimamizi, Utafutaji na usimamizi wa miradi mikubwa na midogo, kuongea lugha mbalimbali, mashirika ya umma na mashirika binafsi. Amewahi kufanya kazi kama  Meneja wa Hazina wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii LAPF. Kupitia uzoefu wake, ameweza kuzisaidia Bodi nyingi kwenye Changamoto ya kifedha na kujiimarisha, kuendesha Biashara kubwa, kusaidia kukuza biashara mpya, na pia ana uwezo wa kuandaa Mpango Mkakakati kwa Maendeleo ya Shirika. Bwana Magambo alipata shahada yake ya kwanza kutoka Hanze University College – Groningen – Uholanzi, Shahada ya Uongozi wa Biashara katika masuala ya Fedha na Uhasibu, na ana shahada ya Uzamivu (Dutch Doctoral Programme – Doctorandus (Drs) - Associate Doctorate and MSc (Economics) – Kitivo cha Uchumi na Uongozi wa Biashara - kutoka Tilburg University - Uholanzi: Julai 2003.

Contact info

TCCIA Investment Company Limited [TICL] is a public limited liability company that was established by shareholders to expand financing sources to participate meaningfully in the ownership and control of the Tanzanian economy