Skip to main content
Mjumbe
Contact Info
Education

Bi Mkocha ana shahada ya Sayansi katika Kilimo kutoka Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam, 1979, na shahada ya Uzamili ya Sayansi katika Kilimo kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine. 1988. Ana uzoefu wa kufanya kazi wa miaka 37. Kutoka Aprili 1979 hadi Juni 2002 aliajiriwa na Shirika la Kilimo na Chakula (NAFCO). Mwezi Julai 2002 alijiunga na Chama cha wafanyabiashara, wenye Viwanda na Kilimo Tanzania kama Afisa Mwandamizi wa Maendeleo wa TCCIA na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Kilimo. Yeye ni mjumbe wa Kamati ya Ukaguzi na Athari za Kampuni. Bi Mkocha ni mjumbe wa Bodi/Kamati zifuatazo:- Baraza la Kazi, Uchumi na Ustawi la Wizara ya Kazi, Bodi ya Nyama Tanzania, Kamati ya Taifa ya Usafi, Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya VETA na mjumbe wa Kamati ya Ufundi ya Ushauri ya Bodi ya Sukari Tanzania. Pia amesajiliwa na Chuo cha Wakurugenzi Tanzania (IoDT).

Contact info

TCCIA Investment Company Limited [TICL] is a public limited liability company that was established by shareholders to expand financing sources to participate meaningfully in the ownership and control of the Tanzanian economy